CHINA YAMUONYA TRUMP JUU YA MANENO YAKE DHIDI YA KOREA KASKAZINI.

Rais Xi Jinping
Rais wa China Xijinping
Rais wa China Xijinping amemtaka rais Donald Trump kuchunga matamshi na vitendo vinavyozidisha hali ya kuzua wasiwasi ,chombo cha habari cha kiserikali kimeripoti.

Rais Trump na Korea Kaskazini wamekuwa wakirushiana cheche za maneno huku rais huyo wa Marekani akionya kuikabili kivita vikali Korea Kaskazini.

Lakini China ambaye ni mshirika mkuu wa Korea Kaskazini ametaka pande zote mbili kuwa na uvumilivu.

Taarifa ya ikulu ya Whitehouse imesema kuwa Marekani na China zilikubaliana kwamba Korea Kaskazini inafaa kusitisha uchokozi na tabia mbaya.

Hofu kubwa inayoendelea kutanda kuhusu mpango wa kinyuklia wa Korea Kaskazini ilizidi baada ya taifa hilo kufanyia majaribio makombora yake ya masafa marefu mnamo mwezi Julai.

No comments

TUFATILIE TWITTER

Powered by Blogger.