Marekani: Korea Kaskazini Haitutishi, Tuna Silaha nzito za Kinyukilia.


Waziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani Rex Tillerson amesema kuwa hakuna tishio lolote la hivi karibuni kutoka Korea Kaskazini , licha ya Pyongyang kusema kuwa inapanga kushambulia eneo la Guam nchini Marekani.

Kuhusu Guam bwana Tillerson pia alimtetea rais Donald Trump ambaye ameitishia Korea Kaskzini kwamba ataikabili kivita.

Alisema kuwa rais Trump alitaka kutuma ujumbe kwa Korea Kaskazini.

Lakini rais huyo amejigamba katika mtandao wa Twitter kuhusu uwezo mkubwa wa zana za kinyuklia za Marekani.

Katika ujumbe wa mtandao wa Twitter uliochapishwa mwendo wa Alfajiri, rais Trump alisema kuwa silaha za kinyuklia za Marekani zimeimarika zaidi ya ilivyokuwa lakini akasema kuwa anatumai hatalazimishwa kuutumia uwezo huo.

No comments

TUFATILIE TWITTER

Powered by Blogger.