ANGEL BERNAD KUTOA WIMBO MPYA


Muimbaji mashuhuri wa nyimbo za injili nchini Tanzania mwanadada Angel Bernard anayefanya vizuri na wimbo wa 'SITEKETEI' na 'JANA LEO' hivi leo amefunguka na kuweka wazi kuwa muda sio mrefu anatoa kitu kipya tena.

Kama wewe ni mfatiliaji wa nyimbo za injili itakuwa unakumbuka tarehe november 21 2017 ndio siku aliotoa wimbo wake wa 'JANA LEO' ambao unafanya vizuri nje na ndani ya nchi ila leo kupitia ukusa wake wa Instagram ameahidi kutoa kigongo kingine hivi punde.



Angel Bernad amewasihi mashabiki zake kukaa mkao wa kula kwa kupokea wimbo huoa huku akisisitiza upo tayari.

"New song alert Watu wa Mungu nawaita ku subscribe kwenye Chanel yangu ya YouTube .A new song ,audio and video is coming very soon na kwa wewe ku subscribe utakuwa wa kwanza kupata notification punde wimbo utokapo." ameandika Angel.



Angel Bernad ni moja kati wa waimbaji wanaojitahidi sana kufanya kazi nzuri na kumtumikia MUNGU sanjari na hayo amekuwa akipenda kwa huduma yake ya uimbaji ambapo wapo wengi wanaotaka kuwa kama yeye, Rose Zefania ni muimbaji pia anavutiwa sana na mwadada huyo kwa kupenda anacho kifanya.

Hebu tazama kazi ya Rose Zefania hapa chini, na yeye pia anandoto za kuwa Angel Bernard wa pili. Ameni
.




Rose anafanya vizuri na albamu yeke inayoitwa nishike mkono


TAZAMA VIDEO KUFAHAMU JINSI MUIMBAJI UNAVYOWEZA KUJITANGAZA NA KUJULIKANA.











No comments

TUFATILIE TWITTER

Powered by Blogger.