ANNASTACIA MUKABWA AMETOA KITU KIPYA ”Watangoja Sana”

Muimbaji wa Nyimbo za injili kutoka Kenya Annastacia Mukabwa
Katika dunia ya leo chuki na uadui baina ya mtu na mtu umekuwa kwa kiasi kikubwa hasa kwa watoto wa Mungu ambao wameamua kumtumikia Yesu katika maisha yao, vita ni kubwa kila unapopiga hatua ya mafanikio lakini leo kupitia mtumishi wa Mungu Annastacia Mukabwa tunakumbushwa kuwa ni Mungu peke yake ndiye mwenye neno la Mwisho juu yako, Hakuna silaha itakayoinuka kinyume chako ifanikiwe, maneno ya watu yasikuvunje moyo tegemea utashinda wanaongoja kuanguka kwako ”Watangoja Sana”.

Kutoka jijini Nairobi Kenya leo nimekuletea video iitwayo Watangoja Sana kutoka kwa mwimbaji mahiri na mkongwe katika kiwanda cha muziki wa Injili nchini humo anayefahamika kwa jina la Annastacia Mukabwa.

Nina imani kuwa utabarikiwa na kuinuliwa kupitia video na wimbo huu, nakukaribisha kutazama na siku zote amini kuwa wewe ni mshindi.. Hakuna Silaha itakayoinuka kinyume chako ifanikiwe.. Ameen!


Kama wewe ni muimbaji unahitaji kufanya Interview na HABARI ZONE MEDIA karibu sana tuwasiliane kwa namba 0768 102 984 AU 0689454357. Asante

Usiache Kufatilia HABARI ZONE media kila siku kuhusu story za wasanii na habari mbali mbali za kijamii, tunapatika Facebook, Twitter, Whatsapp Goup(0768102984) na Instgram.

No comments

TUFATILIE TWITTER

Powered by Blogger.