HII NDIO SIRI YA MAFANIKIO YAKO - MWL MWAMBUNGU
ZINGATIA HAYA.
1)AMUA UNACHOTAKA:Watu wengi sana hawajui kitu wanachokitafuta.Wako bize na maisha ila hawajui wanaenda wapi.
2)ANDIKA:Usiseme nina malengo wakati haujaandika popote.Kuna tofauti kubwa kati ya Matamanio na Malengo.Kuna kitu kikubwa kinatokea unapoandika malengo yako.
3)TENGENEZA MPANGO:Kila unachokitafuta kwenye maisha kuna njia mbalimbali za kukipata.Amua wewe unataka kukipata kwa njia gani.Mpango utahusisha rasilimali unazohitaji(Muda,Fedha,watu n.k).Usiseme tu unachotaka kufanikiwa,andika pia utafaniwaje(How).
4)KILA SIKU FANYA KITU:Mafanikio yako yamefichwa kwenye kufanyia kazi ulichoamua kwenye namba 1.Kila siku fanya kitu hata kama ni kidogo sana,hakikisha siku haipiti haufanyi kitu kuhusiana na lengo lako.
Je,tangu mwaka umeanza kitu gani umezingatia kati ya haya?.
TAZAMA VIDEO KUJUA JINSI MUIMBAJI ANAVYOWEZA KUJITANGAZA NA KUJULIKANA ZAIDI - MWALIMU MWAMBUNGU

Leave a Comment