ROSE ZEFANIA ALILIA KUSHIKWA MKONO

muimbaji wa nyimbo za injili Rose Zefania

Asikwambie mtu hapa duniani mabaya ni mengi, shida zipo za kutosha na majaribu makubwa lakini bila kutengeneza mahusiano mazuri na mwenyezi MUNGU hutaweza kuepushwa na mabaya kamwe.

Mungu ndiye mwokozi wa kila kitu na nikimbilio la wote anawapigania wote ni ngome na nguzo ya kutuepusha na mabaya ya dunia, 
Usiku na mchana tuwe watakatifu hakika tutaepushwa na mabaya ya dunia.

Mwanadada muimbaji wa nyimbo za injili hapa Tanzania kutoka mkoani Kagera Rose Zefania anayefanya vizuri na albamu yake ya 'NISHIKE MKONO' anatukumbusha na kutusihi MUNGU ndiye kimbilio na tusiache kumtumika hapa duniani ili mbinguni atupoke katika ufalme wake.

Albamu hiyo inajumla ya nyimbo saba ambazo ni 
1. NISHIKE MKONO
2. WEMA WAKO
3. BWANA WAWEZA
4. NASHUKURU
5. ROHO MTAKATIFU
6. NAULIZA WALIMWENGU
7. MRUDIE yesu


Karibu kuskiliza na kutazama wimbo wake uliobeba albamu 'NISHIKE MKONO' hakika utabarikiwa kwa ujumbe mzuri. Ameni.



Kwa mawasiliano na muimbaji Rose Zefania unaweza kumpata kupitia Mtandao wa Facebook na Instagram kwa jila la Rose Zefania au kwa namba 075 444 7941.

No comments

TUFATILIE TWITTER

Powered by Blogger.