MANCHESTER UNITED YASONGA MBELE EUROPA LEAGUE.
Manchester United wamesonga mbele na kuingia robo fainali ya michuano ya UEFA Europa League baada ya kuifunga Rostov 1-0 katika mchezo wa raundi ya pili uliochezwa Old Trafford.
United wamesonga mbele kwa jumla ya magoli 2-1.
Juan mata ndio alifunga bao hilo pekee katika mchezo ambao United walionekana kupata tabu kuvunja ngome ya Rostov. Manchester United wangeweza kusonga mbele hata kwa matokeo ya 0-0 kwa kuwa tayari walikuwa na goli la ugenini.
Wasiwasi kwa mashabiki wa Manchester United pengine ni kuumia kwa kiungo wao Paul Pogba ambaye hakumaliza mchezo, kutokana na kuumia msuli wa paja. Nafasi yake ilichukuliwa na Marouane Fellaini.
United walitawala mpira lakini hawakufanikiwa kupata chochote hadi katika dakika ya 70 ambapo Mata alifunga bao hilo la ushindi.
Juan mata ndio alifunga bao hilo pekee katika mchezo ambao United walionekana kupata tabu kuvunja ngome ya Rostov. Manchester United wangeweza kusonga mbele hata kwa matokeo ya 0-0 kwa kuwa tayari walikuwa na goli la ugenini.
Wasiwasi kwa mashabiki wa Manchester United pengine ni kuumia kwa kiungo wao Paul Pogba ambaye hakumaliza mchezo, kutokana na kuumia msuli wa paja. Nafasi yake ilichukuliwa na Marouane Fellaini.
United walitawala mpira lakini hawakufanikiwa kupata chochote hadi katika dakika ya 70 ambapo Mata alifunga bao hilo la ushindi.
Leave a Comment